Pamoja na mwamba migogoro inaweza kuwa chanzo cha mabadiliko chanya, isipotatuliwa kwa ufanisi huwa chanzo cha ukosefu wa maendeleo katika jamii
i. Kijamii: migogoro isitatuliwa kikamilifu imekuwa ndio chanzo cha udhaifu katika utoaji wa huduma za kielimu, afya, maji nk. Aidha husababisha kuvunjika kwa ndoa na watoto wasio na malezi sahihi
ii. Kiuchumi: huathiri biashara, miradi, mgawanyo na mapato pamoja na uzalishaji mali
iii. Kisiasa: huathiri maamuzi, uchaguzi, utekelezaji na mipango ya nchi
Mambo sita ambayo mara nyingi ni kiini cha migogoro
i. Taarifa: taarifa kinzani (contradictory information),taarifa ambazao hazijitoshelezi, taarifa zilizofika kwa kuchelewa
ii. Rasilimali: mgawanyo mbaya wa rasilimali kama vile fedha, muda n.k
iii. Changamoto katika mahusiano: jinsi watu wanavyo tegemeana kama kuna upande mmoja ambao hauridhishwi na mambo fulani n.k
iv. Tofauti katika vipaumbele na mahitaji: mahitaji ambayo mara nyingi yanaleta mgogoro ni kutambuliwa (the need for identity) na heshima (the need for respect)
v. Changamoto katika muundo (structure): nani ana mamlaka na anayatumiaje nani anahisi kutengwa au kudharauliwa
vi. Itikadi na maadili/utamaduni: tofauti katika itikadi na utamaduni zisipochukuliwa vizuri huwezi kusababisha migogoro
Jinsi ya kuchambua vyanzo vya migogoro
Kuna mambo makubwa mitatu ya kuangalia wakati wa kuchambua migogoro:
i. WATU: ni akina nani wanahusika katika migogoro huu, wanahusikaje na nini mchango wao katika migogoro huu?
ii. MCHAKATO: hapa tunaangalia historia ya migogoro wenyewe. Je kuna utaratibu uliokiukwa au kusahaulika ambao ndio umesababisha migogoro> kwa mfano ardhi ya kijiji inapouzwa bila huhusisha wanakijiji mara nyingi huleta ngogoro baadae
iii. TATIZO: watu wanaozozana wanagombania nini? Nini KIINI cha mgogoro huu
Je unahisi kwanini migogoro mingi hujirudia rudia? Comment below

Newspaper is an amazing magazine blogger theme that is easy to use and change to fit your needs
No comments
Post a Comment